Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yesu alipoona namna walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, zambi zako zimesamehewa.”

Gade chapit la Kopi




Marko 2:5
28 Referans Kwoze  

Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.


Kwa maana mumeokolewa kwa neema ya Mungu, kwa njia ya imani. Jambo hili halitokani na ninyi wenyewe, lakini ni zawadi ya Mungu.


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Kisha Yesu akamukuta mutu yule ndani ya hekalu, akamwambia: “Angalia, sasa umepona. Basi usifanye zambi tena, kusudi jambo baya zaidi lisikufikie.”


Yesu alipoona namna walivyomwaminia, akasema: “Rafiki yangu, zambi zako zimesamehewa.”


Muvumiliane na kusameheana ninyi kwa ninyi wakati wowote mutu anapokuwa na neno la kumushitaki mwingine. Munapaswa kusameheana kama vile Bwana alivyowasamehe ninyi.


Wakati munaposamehe mutu, nami ninamusamehe vilevile. Kwa maana kama ninasamehe, na ikiwa kweli ninakuwa na neno lolote la kusamehe, ninasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,


Na kwa sababu hii wengi kati yenu ni wagonjwa na wazaifu, na wengi wamekufa.


Yeye alikuwa akisikiliza mahubiri ya Paulo. Paulo akamukazia macho, naye akaona kwamba kiwete yule yuko na imani ya kuweza kuponyeshwa.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Naye hakuhitaji kupewa ushuhuda juu ya mutu yeyote, kwa maana yeye mwenyewe alijua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu.


Na Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani.”


Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani, ugonjwa wako umepona!”


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Nilipata mateso makali kwa faida yangu; lakini umeyaokoa maisha yangu kutoka shimo la uharibifu, maana umezitupa zambi zangu nyuma yako.


Ananisamehe uovu wangu wote, na kuniponyesha magonjwa yote.


Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


Kitu gani kinachokuwa chepesi kusema: ‘Zambi zako zimesamehewa’, au kusema: ‘Simama, utembee’?


Walimu wamoja wa Sheria walioikaa pale wakajiuliza:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite