Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala nyama wako wa kufugwa, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako.
Na wakati walimu wa Sheria wa kikundi cha Wafarisayo walipomwona Yesu akikula pamoja na watu wale, wakawauliza wanafunzi wake: “Kwa sababu gani anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,
Wageni watakaoshikamana nami Yawe, kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu, na kuwa watumishi wangu, wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua, watu watakaofuata agano langu,
Mutafanya kazi zenu kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba ni siku ya Sabato, ni siku ya kupumzika ambayo ni takatifu kwa ajili ya Yawe. Mutu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo lazima atauawa.