Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 2:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni katika siku zile ndipo watafunga kula.

Gade chapit la Kopi




Marko 2:20
29 Referans Kwoze  

Kisha akawaambia wanafunzi wake: “Kutakuwa siku mutakazotamani kumwona tena Mwana wa Mutu kwa muda tu, lakini hamutapata muda ule.


Kisha mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe vilivyojaa mapigo saba ya mwisho, akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha bibi arusi, muke wa Mwana-Kondoo.”


Tufurahi na kushangilia na kumutukuza, kwa sababu saa ya ndoa ya Mwana-Kondoo imetimia, naye bibi arusi wake amejitayarisha.”


Nimesumbuka kwa kufanya kazi ngumu, nimepata magumu, nimekesha mara nyingi. Mara nyingi niliteswa na njaa na kiu; mara nyingi nililazimishwa kutokula. Nimeteseka na baridi na ukosefu wa nguo.


Mimi ninasikia wivu kwa ajili yenu sawa vile Mungu anavyousikia vilevile. Kwa maana ninyi ni kama binti mukamilifu niliyemwowesha kwa mume mumoja, ndiye Kristo.


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Wakawachagua wazee katika kila kanisa. Na kisha kuomba na kufunga kula chakula, wakawaweka chini ya ulinzi wa Bwana waliyemwamini.


Yeye anapaswa kubaki mbinguni mpaka zitakapotimia zile nyakati Mungu atakapotengeneza vitu vyote sawa vile alivyosema tangu zamani kwa kinywa cha manabii wake watakatifu.


Kisha kusema maneno haya, Yesu akanyanyuliwa mbinguni, nao walikuwa wakimwangalia. Na wingu likamuficha hata hawakumwona tena.


Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Mwenye bibi arusi ndiye bwana-arusi; lakini rafiki ya bwana arusi anasimama karibu naye na kumusikiliza, anafurahi sana kusikia sauti ya bwana-arusi. Na ni hivi mimi ninafurahi, na furaha yangu imetimia sasa.


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Mukuje basi enyi wabinti wa Sayuni, mumwone mufalme Solomono. Amevaa taji aliyovalishwa na mama yake, siku alipofanya ndoa yake, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.


Sikiliza binti, ufikiri! Tega sikio lako: sahau sasa taifa lako na jamaa yako.


Tumepigwa, tumetiwa ndani ya kifungo, wamefanya fujo juu yetu, tumefanya kazi ngumu, tumekoseshwa usingizi na kukaa bila kula.


Mutakuwa na wamasikini pamoja nanyi siku zote, lakini hamutakuwa nami siku zote.”


Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba warafiki za bwana-arusi wanaweza kufanya kilio wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao; ni siku zile watafunga kula.


Yesu akawajibu: “Munafikiri kwamba wanaoalikwa kwa arusi wanaweza kujizuiza kula chakula cha karamu wakati bwana-arusi angali pamoja nao? Hapana! Wakati bwana-arusi angali pamoja nao hawawezi kujizuiza kula.


“Hakuna mutu anayeshonea kiraka kipya juu ya nguo ya zamani. Kama akifanya vile, kile kiraka kipya kinapasua nguo ya zamani, nako kupasuka kwake kunaongezeka zaidi.


Lakini kutakuwa siku bwana-arusi atakapoondoshwa kati yao. Katika siku zile ndipo watafunga kula.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite