Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 16:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Nao wote watakaoniamini watafanya vitambulisho hivi: watafukuza pepo kwa jina langu; watasema kwa luga mupya;

Gade chapit la Kopi




Marko 16:17
17 Referans Kwoze  

Watu wengi vilevile kutoka miji inayokuwa pembeni ya Yerusalema walikusanyika, wakiwaleta wagonjwa na watu wanaoteswa na pepo, na wote wakaponyeshwa.


Vilevile Mungu ameweka kwanza mitume katika kanisa; pili manabii na tatu walimu; kisha kunakuwa wale wenye zawadi ya kufanya miujiza, ya kuponyesha wagonjwa, ya kusaidia wengine, ya kuongoza wengine, ya kusema luga za ajabu.


Mwingine anapewa uwezo wa kufanya miujiza, mwingine zawadi ya kutabiri, na mwingine uwezo wa kutambua roho ya uongo na Roho wa ukweli. Mwingine alipewa uwezo wa kusema luga za ajabu na mwingine uwezo wa kutafsiri luga zile.


Maana pepo walitoka ndani ya watu wengi wakilalamika kwa sauti kubwa, na watu wengi wenye kupooza pamoja na viwete waliponyeshwa vilevile.


Wale wanafunzi makumi saba wakarudia wakijazwa na furaha, nao wakasema: “Bwana, hata pepo wanatutii tunapowaamuru kwa jina lako!”


Kwa maana waliwasikia wakisema kwa luga za ajabu na kumutukuza Mungu. Halafu Petro akasema:


Kweli, kweli ninawaambia: yeye anayeniamini atafanya vilevile matendo ninayofanya. Na zaidi ya ile atafanya matendo makubwa kuliko haya, kwa sababu ninakwenda kwa Baba.


Paulo akaweka mikono yake juu yao, na Roho Mutakatifu akashuka juu yao, nao wakaanza kusema kwa luga na kutabiri.


Mutu anayesema kwa luga ya ajabu hasemi na watu lakini anasema na Mungu, kwa maana hakuna mutu anayemusikia. Kwa uwezo wa Roho, mutu yule anasema mafumbo.


wa kuponyesha wagonjwa, wa kusema kwa luga za ajabu, au wa kutafsiri.


Hata nikiwa na uwezo wa kusema luga za watu na za wamalaika, lakini kama sina upendo, masemi yangu ni bure kama vile kelele la kengele au matoazi.


Naye akafanya hivi kwa muda wa siku nyingi. Na kwa mwisho Paulo akachukizwa naye. Basi akageuka na kumwambia yule pepo: “Ninakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, utoke ndani yake!” Na saa ile ile yule pepo akatoka ndani yake.


Yoane akamwambia Yesu: “Mwalimu, tulimwona mutu mumoja akifukuza pepo kwa jina lako, nasi tulimukataza kwa sababu yeye si wa kikundi chetu.”


Na kisha kunyanyuliwa aikae na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Baba yake, yeye akamupa Roho Mutakatifu aliyeahidiwa. Naye akamushusha juu yetu, sawa vile munavyojionea na kusikia wenyewe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite