Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 15:46 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

46 Yosefu akanunua vitambaa, akaondoa maiti ya Yesu juu ya musalaba, akaifungafunga na vile vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa ndani ya jiwe. Kisha wakasukumia jiwe kwenye kiingilio cha lile kaburi.

Gade chapit la Kopi




Marko 15:46
12 Referans Kwoze  

Walimuzika pamoja na waovu; katika kifo aliwekwa pamoja na watajiri, ingawa hakutesa watu hata kidogo, wala hakusema neno lolote la udanganyifu.


Basi Yesu akasisimua tena kwa huzuni, na kwenda kwenye kaburi. Kaburi lile lilikuwa pango lililofungwa na jiwe kubwa.


Una haki gani kuwa huku? Una ndugu yeyote hapa, hata ukajichongea kaburi ndani ya jiwe juu ya mulima?


Alipokwisha kuishusha toka juu ya musalaba, akaifungafunga na vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa katika jiwe. (Ndani ya kaburi lile mulikuwa bado hamujazikwa mutu.)


Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.


Alipokwisha kuhakikishwa na yule mukubwa wa waaskari kwamba Yesu amekwisha kufa, akamuruhusu Yosefu atwae maiti yake.


Maria wa Magdala na Maria mama ya Yose walikuwa wakiangalia, pahali walipomuzika Yesu.


Basi wakaondosha lile jiwe. Yesu akainua macho juu, akasema: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia.


Siku ya kwanza ya juma asubui mapema, kulipokuwa kungali giza, Maria wa Magdala akaenda kwenye kaburi. Alipofika kule akaona kama jiwe lililofunika kaburi limeondolewa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite