Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 15:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.

Gade chapit la Kopi




Marko 15:32
16 Referans Kwoze  

Hata wale wanyanganyi waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.


Hao wamepotoka mbali na ukweli, wamepotosha imani ya watu wengi wakisema kwamba ufufuko tunaongojea umekwisha kufanyika.


Hivi hesabu ya vizazi vyote tangia Abrahamu mpaka Daudi ni vizazi kumi na vine, na tangia Daudi mpaka Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli ni vizazi kumi na vine, na tangia Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli mpaka kuzaliwa kwa Kristo ni vizazi kumi na vine.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yawe amekuondolea hukumu iliyokuwa juu yako, amewafukuza waadui zako. Yawe, mufalme wa Israeli yuko pamoja nawe. Hautaogopa tena hasara.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Tuseme nini basi? Ikiwa wamoja kati yao hawakukuwa waaminifu, jambo hilo litaweza kuonyesha kwamba Mungu ataacha kuwa mwaminifu?


Basi wakatwaa matawi ya ngazi na kwenda kumupokea, wakilalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Abarikiwe mufalme wa Waisraeli!”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Na tangazo hili liliandikwa kwa kuonyesha sababu ya kuhukumiwa kwake. “Mufalme wa Wayuda.”


“Aliokoa wengine, lakini sasa anashindwa kwa kujiokoa yeye mwenyewe! Yeye ni mufalme wa Waisraeli, sasa ajishushe pale juu ya musalaba kusudi nasi tupate kumwamini.


Vilevile waliwatundika wanyanganyi wawili juu ya misalaba pamoja na Yesu, mumoja kwa upande wake wa kuume na mwingine kwa upande wa kushoto. [


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite