Marko 15:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
32 Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.” Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.
Hivi hesabu ya vizazi vyote tangia Abrahamu mpaka Daudi ni vizazi kumi na vine, na tangia Daudi mpaka Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli ni vizazi kumi na vine, na tangia Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli mpaka kuzaliwa kwa Kristo ni vizazi kumi na vine.
Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.
Basi wakatwaa matawi ya ngazi na kwenda kumupokea, wakilalamika kwa sauti kubwa, wakisema: “Mungu asifiwe! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Abarikiwe mufalme wa Waisraeli!”
“Aliokoa wengine, lakini sasa anashindwa kwa kujiokoa yeye mwenyewe! Yeye ni mufalme wa Waisraeli, sasa ajishushe pale juu ya musalaba kusudi nasi tupate kumwamini.