Marko 15:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Mutu mumoja wa Kurene, aliyeitwa Simoni, baba ya Alesanduro na Rufu, alikuwa akipita katika njia, akitoka kwenye vijiji. Waaskari wakamushurutisha abebe musalaba wa Yesu.
Nao walipokuwa wakimupeleka Yesu kwenda kutundikwa, wakakutana na mutu mumoja aliyeitwa Simoni, wa inchi ya Kurene, aliyekuwa akitoka kwenye vijiji. Wakamulazimisha abebe musalaba wa Yesu na kumufuata nyuma.
Katika kanisa la Antiokia kulikuwa manabii na walimu wamoja. Kati yao kulikuwa Barnaba, Simoni aliyeitwa vilevile Nigeri; Lukio wa Kurene, Saulo na Manaeni, aliyekomaa pamoja na mufalme Herode.
Lakini kulitokea wanafunzi wengine, waliokuwa watu wa Kipuro na wa inchi ya Kurene, waliofika Antiokia. Nao wakaanza kusemezana na Wagriki vilevile, wakiwahubiri Habari Njema juu ya Bwana Yesu.
Lakini kukatokea watu wamoja waliopingana na Stefano. Watu hawa walikuwa wa nyumba ya kuabudia iliyojulikana kwa jina la “Wenye Uhuru.” Nao walitoka katika inchi ya Kurene na ya Alesanduria, na kutoka jimbo la Kilikia na la Azia. Watu hawa wakaanza kubishana na Stefano