Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 14:65 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

65 Wengine katikati yao wakaanza kumutemea Yesu mate, wakamufunika uso na kumupiga ngumi, wakimwambia: “Tambua sasa ni nani aliyekupiga!” Nao waaskari walinzi wakamukamata Yesu na kumupiga makofi.

Gade chapit la Kopi




Marko 14:65
17 Referans Kwoze  

Paulo aliposema maneno hayo, Kuhani Mukubwa Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wamupige kofi kwenye kinywa.


Wakafika kila wakati mbele yake na kusema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda.” Nao wakamupiga makofi.


Wale walionipiga, niliwaelekezea mugongo wangu, wale walioziongoa ndevu zangu, mashavu yangu. Sikuficha uso wangu wakati watu waliponitukana na kunitemea mate.


Yesu aliposema maneno haya, mumoja wa walinzi waliokuwa karibu naye, akamupiga kofi, akisema: “Ni hivi unavyopaswa kumujibu Kuhani Mukubwa?”


Wakamupigapiga tete juu ya kichwa, wakamutemea mate, wakapiga magoti na kuinama mbele yake.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Wengi waliomwona walishituka, kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika; hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!


Wananichukia na kuniepuka; wakiniona tu wanatema mate kwenye uso.


Kisha mufalme akarudi kutoka katika bustani, na mara alipoingia ndani ya chumba walimokuwa wanakunywa divai, akamukuta Hamani amejitupa karibu na kiti ambamo Esteri alikuwa ameikaa. Kuona hivyo, mufalme akasema kwa sauti kubwa: “Hivi mutu huyu anataka kumushika kwa nguvu malkia mbele yangu, tena ndani ya nyumba ya kifalme?” Mara tu mbele mufalme hajamaliza kusema, matowashi wakamufunika Hamani uso.


Lakini Yawe akamwambia Musa: Kama baba yake angemutemea mate kwenye uso, basi, hangepata haya kwa siku saba? Basi, umutoe inje ya kambi akae kule muda wa siku saba, kisha unaweza kumuruhusu arudi katika kambi.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Nao watamuchekelea, watamutemea mate, watamupiga fimbo na kumwua. Lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.”


Yawe anasema hivi: Lakini wewe Betelehemu katika Efurata, wewe ni mudogo tu kati ya ukoo wa Yuda, lakini kwako kutanitokea mutawala atakayetawala juu ya Israeli. Asili yake ni ya zamani sana.


Kisha nabii Zedekia mwana wa Kenana akamukaribia Mikaya, akamupiga kofi kwenye shavu na kumwuliza: “Kwa njia gani Roho wa Yawe ameniacha na akakuja kusema nawe?”


Wakamutemea mate, wakatwaa lile tete na kumupiga nalo juu ya kichwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite