64 Mumesikia wenyewe jinsi alivyomutukana Mungu. Munawaza nini?” Wote wakamuhukumu kwamba anastahili kufa.
Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe.
Wayuda wakamujibu: “Kufuatana na moja ya sheria zetu, mutu huyu anapaswa kuuawa, kwa sababu alijiita Mwana wa Mungu.”
Kwa ajili ya neno hili Wayuda walitaka tena zaidi kumwua; si kwa sababu ya kuvunja Sheria ya siku ya Sabato tu, lakini vilevile kwa sababu alisema kwamba Mungu ni Baba yake, akijifanya hivi kuwa sawasawa na Mungu.
Halafu wakasema: “Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Kwa maana tunatoka kusikia maneno aliyosema!”
“Kama mutu amefanya kosa linalomupasa auawe na akiuawa kwa kutundikwa juu ya muti,