Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 14:58 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

58 “Sisi tulimusikia akisema: ‘Mimi nitabomoa hekalu hili lililojengwa na watu, na katika siku tatu nitajenga lingine lisilojengwa na watu.’ ”

Gade chapit la Kopi




Marko 14:58
11 Referans Kwoze  

Lakini Kristo alikuja kuwa Kuhani Mukubwa anayeshugulika na mambo mema ambayo sasa yamekwisha kutokea. Yeye alipita katika hema inayokuwa bora zaidi na kamilifu. Hema hii haikutengenezwa na watu, maana yake si ya dunia hii.


Kwa maana, tunajua kwamba hema hii tunayoishi ndani yake hapa katika dunia, maana yake mwili wetu, itakapobomolewa, Mungu atatupatia makao mengine mbinguni. Nayo ni nyumba aliyoijenga yeye mwenyewe na inayodumu milele.


Yesu akawajibu: “Mubomoe hekalu hili, nami nitalijenga katika siku tatu.”


Kwa maana Kristo hakuingia katika Pahali Patakatifu palipojengwa na watu, panapokuwa tu mufano wa Pahali Patakatifu kamili, lakini aliingia katika mbingu yenyewe, pahali anaposimama sasa mbele ya Mungu kwa kututetea.


“Lakini Mungu Mukubwa hakai ndani ya nyumba zilizojengwa na watu kama vile inavyosemwa katika maandiko haya ya manabii:


Watu waliokuwa wakipita pale walimutukana na kutikisatikisa vichwa vyao, wakisema: “Ewe! Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu,


Ulipokuwa ukiangalia, jiwe liliongoka lenyewe, bila kuguswa, na kuipondaponda miguu ya shaba na udongo wa mufinyanzi ya ile sanamu, na kuivunja vipandevipande.


Uliliona jiwe lililoongoka lenyewe toka kwenye mulima, bila kuguswa, na jinsi lilivyoivunja vipandevipande ile sanamu iliyotengenezwa kwa chuma, shaba, udongo wa mufinyanzi, feza na zahabu. Ee mufalme, Mungu Mukubwa amekufunulia mambo yatakayotukia nyuma. Ni mimi ninayekuelezea hivyo. Ndoto yako ni ya kweli na maana yake ni ya kuaminiwa.


na kusema: “Mutu huyu alisema kwamba anaweza kubomoa hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa muda wa siku tatu.”


Hata wengine wakasimama kwa kutoa ushuhuda huu wa uongo juu yake wakisema:


Lakini hata hivi ushuhuda wao haukupatana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite