Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ninyi wote mutaanguka, kwa maana imeandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo watasambazwa.’
Kutakuwa wakati, nao umetimia, ndio wakati mutakaposambazwa, kila mutu akijiendea ngambo yake mwenyewe, nanyi mutaniacha peke yangu. Lakini mimi si peke yangu kabisa, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.
Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”