Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 14:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”

Gade chapit la Kopi




Marko 14:49
27 Referans Kwoze  

Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.


Na kesho yake asubui mapema akarudi tena katika hekalu. Watu wote wakamufikia, naye alipoikaa, akaanza kuwafundisha.


Kwa maana ninawaambia, ni lazima yatimie kwangu maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: ‘Naye alihesabiwa pamoja na watenda maovu.’ Kwa sababu yanayonielekea mimi yanafikia kwa mwisho wake.”


Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu akauliza: “Namna gani walimu wa Sheria wanaweza kusema kwamba Kristo ni Mwana wa Daudi?


Mambo haya yote yamefanyika kusudi maneno yanayosemwa na manabii katika Maandiko Matakatifu yapate kutimia.” Basi wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Lakini namna gani yangetimia Maandiko Matakatifu yanayosema kwamba mambo haya yanapaswa kuwa hivi?”


Mambo hayo yote yalitukia kusudi yatimie maneno Bwana aliyosema kwa njia ya nabii:


Yesu alikuwa akitembea ndani ya hekalu katika baraza iliyoitwa baraza ya Solomono.


Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Siku ya mwisho ya sikukuu ile iliyokuwa siku kubwa, Yesu akasimama na kusema hivi kwa sauti: “Mutu akiwa na kiu, akuje kwangu akunywe.


Yesu alikuwa akifundisha kila siku ndani ya hekalu. Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wakubwa wa watu wakatafuta kumwua.


Yesu na wanafunzi wake wakafika tena Yerusalema. Yesu alipokuwa akitembea katika hekalu, wakubwa wa makuhani, walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu, wakamufikia.


Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.


Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.


Kisha Yesu akawaambia: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi?


Wanafunzi wake wote wakamwacha na kukimbia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite