Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.
Yuda akamujibu: “Tukuambie nini bwana? Tuseme nini kwa kuonyesha kwamba hatuna kosa? Mungu ameyafichua makosa yetu, sisi watumishi wako. Sasa sisi wote tuko watumwa wako, sisi pamoja na yule aliyepatikana na kikombe chako.”
Aliporudi kwa mara ya tatu, akawaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Inatosha! Saa imetimia. Sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.
Kwa wakati ule Petro na wenzake walikuwa wamewezwa sana na usingizi; lakini wakaamuka, wakaona ule utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wakisimama pamoja naye.