17 Ilipokuwa magaribi, Yesu akafika pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
Saa ilipotimia, Yesu akaikaa kula chakula pamoja na wanafunzi wake.
Halafu wanafunzi wakaondoka, wakaenda katika muji, wakakuta vitu vyote tayari sawa vile Yesu alivyowaambia. Nao wakatayarisha karamu ya Pasaka.
Walipokuwa wameikaa kula chakula, Yesu akasema: “Kweli ninawaambia: mumoja kati yenu anayekula pamoja nami atanitoa.”
“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’