Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 14:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Naye atawaonyesha chumba kikubwa cha gorofi, kilichokwisha kupangwa vizuri na kuwa tayari. Ni mule mutakapotutayarishia karamu.”

Gade chapit la Kopi




Marko 14:15
12 Referans Kwoze  

Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Na kulikuwa taa nyingi katika chumba cha gorofi tulichokusanyika ndani yake.


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Mwanadamu anapanga mipango yake, lakini neno la mwisho ni la Yawe.


Watu wako watajitolea, siku utakapokwenda kuwapiga waadui. Juu ya milima mitakatifu vijana wako watakufikia, kama umande unaotokeza asubui mapema.


basi usikilize kutokea kule mbinguni, utoe musamaha, vilevile umutendee kila mutu kadiri anavyostahili, (maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote),


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


na pahali atakapoingia, mumwambie mwenye nyumba: ‘Mwalimu anauliza kwamba ni wapi kunapokuwa chumba chake ambamo atakulia karamu ya Pasaka pamoja na wanafunzi wake.’


Halafu wanafunzi wakaondoka, wakaenda katika muji, wakakuta vitu vyote tayari sawa vile Yesu alivyowaambia. Nao wakatayarisha karamu ya Pasaka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite