37 Mambo ninayowaambia ninyi, ninayasema kwa wote: mukeshe.”
Mujiangalie, mukeshe, kwa maana hamujui saa wakati ule utakapotimia.
Basi muangalie sababu hamujui wakati bwana wa nyumba atakaporudi: labda magaribi, au katikati ya usiku, au wakati jogoo anapowika, au asubui.
Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku Bwana wenu atakaporudi.
Mufanye vile, maana munajua tunaishi katika siku gani sasa. Saa ya kuamuka katika usingizi wenu imetimia, kwa maana sasa wakati wetu wa kuokolewa unakaribia kuliko vile ilivyokuwa wakati tulipoanza kuamini.