Marko 13:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
34 Itakuwa kama vile mutu anayefunga safari. Alipotoka kwake akawaachia watumishi madaraka yake, akimupa kila mutu kazi yake. Vilevile akamwagiza mulinzi wa mulango akeshe.
Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.
Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni; chochote utakachokikataza katika dunia, kitakatazwa mbinguni vilevile, na chochote utakachokiruhusu katika dunia, kitaruhusiwa mbinguni vilevile.”
“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.