Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 13:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Mujiangalie, mukeshe, kwa maana hamujui saa wakati ule utakapotimia.

Gade chapit la Kopi




Marko 13:33
19 Referans Kwoze  

Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Kwa hiyo ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudia saa musiyozania.”


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


Mukuwe waangalifu na mukeshe, kwa maana adui yenu Shetani anazungukazunguka kama simba anayenguruma akitafuta yule atakayerarua.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.


Amuka! Uimarishe kile kinachobaki kinachokaribia kufa, kwa maana nimeona kwamba matendo yako si makamilifu mbele ya Mungu wangu.


Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.


Lakini ninyi mujiangalie vizuri, kwa maana nimewaambia hayo yote mbele.


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.


Mudumu katika kuomba. Munapoomba mukeshe na kumutolea Mungu shukrani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite