Yesu akaikaa akielekea kwenye sanduku ya kutilia sadaka za hekalu. Akaangalia jinsi watu walivyotia feza ndani ya sanduku ile. Watajiri wengi walitia feza nyingi ndani yake.
Basi Yesu akawaita wanafunzi wake na kuwaambia: “Kweli ninawaambia kwamba mujane huyu masikini ametoa mingi zaidi kuliko wote wanaotia feza ndani ya sanduku ya sadaka.
Na yeyote atakayetoa hata kikombe kimoja tu cha maji ya baridi kwa mumoja wa hao wanaokuwa wadogo kati ya wanafunzi wangu, kwa sababu yeye ni mwanafunzi wangu, kweli ninawaambia: mutu yule hatakosa kupewa zawadi yake.”
Yalijaribiwa sana kwa njia ya mateso mengi yaliyopata. Lakini yalizidi kuwa na furaha hata yakakuwa na moyo wa kutoa kupita kipimo, ingawa yalikuwa masikini sana.
Kwa maana kama mutu akiwa na moyo wa kutoa, Mungu anakubali kitu anachotoa kufuatana na kile anachokuwa nacho, wala si kufuatana na kile asichokuwa nacho.