Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.
Yesu akamujibu: “Nilisema na watu wote waziwazi, nilifundisha siku zote katika nyumba za kuabudia na katika hekalu, pahali Wayuda wote wanapokutana. Sikusema kitu kwa uficho.
Siku moja Yesu alikuwa katika hekalu akiwafundisha watu na kuhubiri Habari Njema. Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu wakamufikia na kumwuliza:
Yesu na wanafunzi wake wakafika tena Yerusalema. Yesu alipokuwa akitembea katika hekalu, wakubwa wa makuhani, walimu wa Sheria pamoja na wasimamizi wa watu, wakamufikia.
Yesu akaondoka kule, akaenda katika jimbo la Yudea na kuvuka ngambo ingine ya Yordani. Na makundi mengi ya watu wakakusanyika tena mbele yake, naye akaanza kuwafundisha, kama vile alivyozoea kufanya.
Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”