Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 12:33 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

33 Na mutu anapaswa kumupenda Mungu kwa moyo wake wote, kwa akili yake yote na kwa nguvu yake yote, naye anapaswa kumupenda mwenzake kama vile anavyojipenda mwenyewe. Mambo hayo ni bora zaidi kuliko kumutolea Mungu nyama za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine zote.”

Gade chapit la Kopi




Marko 12:33
15 Referans Kwoze  

Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


Mungejua maana ya Maandiko haya Matakatifu, yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu,’ hamungehukumu watu hawa wasiokuwa na kosa.


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Anayenitolea shukrani kama sadaka yake, huyo ndiye anayenitukuza; yeyote anayedumu katika njia yangu, huyo ndiye nitakayemwokoa.”


Kwanza Kristo alisema: “Haukutaka wala haukupendezwa na sadaka na matoleo, wala sadaka za kuteketezwa kwa moto wala sadaka za kusamehewa zambi.” (Alisema vile ingawa sadaka hizo zote zilitolewa kufuatana na maagizo ya Sheria.)


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite