Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 12:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Mwalimu mumoja wa Sheria alikuwa pale Yesu alipobishana na Wasadukayo. Yeye alitambua kwamba Yesu aliwajibu vizuri. Basi akamujongelea na kumwuliza: “Ni amri gani inayokuwa ya kwanza katikati ya amri zote?”

Gade chapit la Kopi




Marko 12:28
8 Referans Kwoze  

Walimu wamoja wa Sheria wakasema: “Mwalimu, umejibu vizuri!”


Naye akauliza: “Amri gani?” Yesu akamujibu: “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,


Ni kwa hiyo mutu yeyote atakayevunja hata amri moja inayokuwa ndogo kuliko zingine zote, na kuwafundisha watu wengine kufanya kama yeye, huyu atahesabiwa kuwa mudogo katika Ufalme wa mbinguni. Lakini yule atakayezishika na kuzifundisha wengine, huyu atahesabiwa kuwa mukubwa katika Ufalme wa mbinguni.


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula, lakini mumeacha mambo makubwa yanayoamuriwa na Sheria, kama vile haki, huruma, na uaminifu. Mambo hayo ndiyo muliyopaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Waliporudi kwenye wanafunzi wengine, wakaona kundi la watu wengi wakiwazunguka na walimu wa Sheria wakibishana nao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite