Marko 12:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
15 Lakini kwa kuwa Yesu alitambua kwamba wao ni wanafiki, akawaambia: “Sababu gani munanipima? Muniletee kikoroti kimoja cha feza hapa kusudi nikione.”
Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.
Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.
Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”
Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.
Walipomufikia, wakamwuliza: “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mutu wa kweli. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu lakini unafundisha kwa ukweli njia Mungu anayoamuru kufuata. Utuambie basi, Sheria inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana? Ni sherti tulipe au hapana?”