Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 12:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini kwa kuwa Yesu alitambua kwamba wao ni wanafiki, akawaambia: “Sababu gani munanipima? Muniletee kikoroti kimoja cha feza hapa kusudi nikione.”

Gade chapit la Kopi




Marko 12:15
14 Referans Kwoze  

Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


Vilevile tusimupime Bwana kama vile wamoja wao walivyofanya, hata wakauawa na nyoka.


Halafu Petro akamwambia: “Namna gani mulipatana kwa kumupima Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale wanaotoka kumuzika mume wako wamefika hapa kwenye mulango, nao watakupeleka vilevile.”


Kisha Yesu akamwuliza mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Basi Petro akauzika kwa sababu Yesu alimwuliza mara ya tatu kama anamupenda. Kwa hiyo akamujibu: “Bwana, unajua yote; unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia: “Tunza kondoo wangu.


Lakini kwa kuwa Yesu alitambua udanganyifu wao, akawaambia:


Wafarisayo wamoja wakamufikia kwa kumupima, wakamwuliza: “Sheria yetu inamuruhusu mutu kufukuza muke wake?”


Lakini kwa kuwa Yesu alijua makusudi yao mabaya, akawajibu: “Ninyi wanafiki, kwa sababu gani munanipima?


Wewe mwanadamu! Tega kitendawili, uwaambie Waisraeli fumbo.


Akapatana na watumishi wamoja kuwalipa kila mutu kikoroti kimoja cha feza sawa na kawaida, naye akawatuma katika shamba lake.


Walipomufikia, wakamwuliza: “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mutu wa kweli. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu lakini unafundisha kwa ukweli njia Mungu anayoamuru kufuata. Utuambie basi, Sheria inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana? Ni sherti tulipe au hapana?”


Wakakileta kwake. Yesu akawauliza: “Sura hii na jina hili linaloandikwa hapa ni vya nani?” Wakamujibu: “Ni vya Mufalme wa Roma.”


Wao walisema hivi kwa kumupima, kusudi wapate sababu ya kumushitaki. Lakini Yesu akainama na kuandika juu ya udongo kwa kidole chake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite