Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 11:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Vilevile hatuwezi kusema kama yalitoka kwa watu…” (Waliogopa kundi la watu kwa maana wote walisadiki kama Yoane alikuwa nabii wa kweli).

Gade chapit la Kopi




Marko 11:32
15 Referans Kwoze  

Basi hao wakubwa wakatafuta kumukamata Yesu, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao. Lakini kwa sababu waliogopa kundi la watu, wakamwacha ajiendee.


Kwa hiyo wakatafuta kumukamata, lakini waliogopa makundi ya watu kwa sababu wao walisadiki kwamba yeye ni nabii.


Herode alitaka kumwua Yoane, lakini aliwaogopa watu kwa maana wote walimuhesabia Yoane kuwa nabii.


Basi mukubwa wa walinzi wa hekalu akaenda pamoja na watumishi wake, akawaleta mitume. Lakini hawakuwakamata kwa kinguvu kwa sababu waliogopa watu wasiwatupie mawe.


Watu wengi wakamufikia na kusema: “Yoane hakuonyesha hata kitambulisho kimoja, lakini maneno yote aliyoyasema juu ya mutu huyu yalikuwa ya kweli.”


Wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria walitafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliogopa watu.


Saa ile ile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria wakatafuta kumukamata, kwa sababu walitambua kwamba alisema mufano huo juu yao.


Herode alimwogopa Yoane, kwa sababu alijua kwamba Yoane ni mwenye haki na mutakatifu. Kwa hivi alimulinda. Alipenda kumusikiliza, ijapokuwa alifazaika sana kila mara alipomusikia.


Basi mulikwenda kuona nini? Nabii? Ndiyo, ninawaambia, yeye ni mukubwa kupita hata nabii.


Nao wakaanza kupiga mafikiri pamoja na kusema: “Kama tukijibu kwamba mamlaka yake yalitoka kwa Mungu, atatuuliza: ‘Kwa sababu gani hamukumwamini?’


Basi wakamujibu Yesu: “Hatujui.” Naye akawaambia: “Nami vilevile sitawaambia ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite