Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 10:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 Watu wengi walimukaripia na kumwambia anyamaze, lakini alizidi kulalamika akisema: “Yesu Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”

Gade chapit la Kopi




Marko 10:48
15 Referans Kwoze  

Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Watu waliotangulia wakamukaripia na kumunyamazisha, lakini alizidi kulalamika, akisema: “Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema maneno haya, wajumbe wakafika kutoka kwa yule mukubwa wa nyumba ya kuabudia na kumwambia: “Binti yako amekwisha kufa. Basi kwa sababu gani ungali unamusumbua Mwalimu?”


Kundi la watu wakawakaripia na kuwaambia wanyamaze. Lakini wale vipofu wakaendelea kulalamika kwa nguvu, wakisema: “Mwana wa Daudi, utusikilie huruma!”


Watu wamoja walimuletea Yesu watoto kusudi awawekee mikono na kuwaombea, lakini wanafunzi wakawakaripia watu wale.


Mutanitafuta mimi na kuniona. Mutakaponitafuta kwa moyo wote,


Mungu amesema mara na mara, nami nimesikia tena na tena kwamba uwezo ni wa Mungu.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Yesu akaondoka toka pale, naye alipokuwa katika njia, vipofu wawili wakamufuata wakilalamika, wakisema: “Utuhurumie, Ee Mwana wa Daudi!”


Watu wamoja wakamuletea Yesu watoto kusudi awawekee mikono, lakini wanafunzi wake wakawakaripia watu wale.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite