Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 10:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Nao wakamujibu: “Tunaweza.” Yesu akaongeza kuwaambia: “Hakika mutakunywa kikombe nitakachokunywa, na kubatizwa kama vile nitakavyobatizwa.

Gade chapit la Kopi




Marko 10:39
10 Referans Kwoze  

Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Akaamuru Yakobo, ndugu ya Yoane, auawe kwa upanga.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Mimi nimetangaza neno lako kwao, na dunia imewachukia kwa sababu wao si wa dunia, kama vile mimi nisivyokuwa wa dunia.


Mukumbuke maneno niliyowaambia kwamba mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake. Kama walinitesa mimi, watawatesa ninyi vilevile. Na kama walishika maneno yangu, watashika maneno yenu vilevile.


Petro akamwuliza: “Bwana, sababu gani siwezi kukufuata sasa? Mimi ni tayari kutoa maisha yangu kwa ajili yako!”


Akasema: “Ee baba! Yote yanawezekana kwako; ninakuomba uniondolee mbali hiki kikombe cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Lakini Petro akazidi kusema kwa nguvu: “Hata ikinipasa kufa pamoja nawe, sitakukana hata kidogo.” Na wote wengine wakasema sawasawa naye.


Lakini inatosha kwa mwanafunzi kufanana na mwalimu wake na mutumishi kufanana na bwana wake. Ikiwa wanamwita mukubwa wa jamaa Belzebuli, hawatakosa kuwaita watu wa jamaa yake kwa majina mabaya zaidi.


Waliungama zambi zao, naye Yoane aliwabatiza katika muto Yordani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite