Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 10:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Wanafunzi wakashangaa sana kusikia maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena: “Watoto wangu, ni vigumu kabisa kuingia katika Ufalme wa Mungu!

Gade chapit la Kopi




Marko 10:24
28 Referans Kwoze  

Anayetegemea mali zake ataanguka, lakini mwenye haki atastawi kama jani bichi.


Wewe unajidai kwamba uko tajiri mwenye mali mengi, wala haukosewi kitu. Lakini haujui kwamba wewe ni mukosefu, mwenye taabu, masikini, kipofu na mwenye kuwa uchi.


Uwaagize wale wanaokuwa watajiri katika dunia hii ya sasa wasijivune, vilevile wasiweke matumaini yao katika mali inayotoweka upesi. Lakini wamutumainie Mungu anayetupatia vitu vyote kwa uwingi kusudi tufurahiwe navyo.


Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele, atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako; atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


Tajiri anazani kwamba mali ni makimbilio yake; anafikiri hayo ni ukuta murefu unaomulinda.


Wanadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Wakipimwa wote pamoja, pumzi ni nzito kuliko wao.


Watoto wangu wapendwa, ninawaandikia maneno hayo kusudi musitende zambi. Lakini kama mutu akitenda zambi, tuko na yule anayetutetea mbele ya Baba. Naye muteteaji yule ndiye Yesu Kristo, mwenye haki.


Watoto wangu, ningali pamoja nanyi kwa muda mufupi tu. Mutanitafuta, lakini sawasawa nilivyowaambia Wayuda, ninawaambia ninyi vilevile kwamba hamuwezi kufika pahali ninapokwenda.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine, unayejenga nyumba yako juu katika milima ukizani kuwa salama mbali na hasara.


Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.


Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona, nao utatoweka mara moja. Maana hakika utajiri unaota mabawa, unaruka na kutoweka katika anga kama tai.


Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.


Watoto wangu wapendwa, muepuke kuabudu sanamu za miungu.


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Watoto wangu wapendwa, kama vile mwanamuke anavyopata uchungu wa kuzaa, mimi vilevile, ninapata tena uchungu kwa ajili yenu mpaka mutakapokuwa na hali inayokuwa kama ya Kristo ndani yenu.


Basi Yesu akawauliza: “Watoto wangu, mumepata samaki?” Wakamujibu: “Hapana.”


Wengi kati ya wanafunzi wake waliposikia maneno haya, wakasema: “Masemi haya ni magumu. Ni nani anayeweza kuyakubali?”


Wanafunzi waliposikia maneno haya, wakashangaa sana na kuuliza: “Ni nani basi anayeweza kuokolewa?”


Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”


Yesu akaangalia pande zake zote na kuwaambia wanafunzi wake: “Kweli ni vigumu sana kwa watajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite