Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 10:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Yesu alipoondoka kwa kuendelea na safari yake, mutu mumoja akamufikia mbio akapiga magoti mbele yake na kumwuliza: “Mwalimu mwema, nifanye nini kusudi nipate kurizi uzima wa milele?”

Gade chapit la Kopi




Marko 10:17
28 Referans Kwoze  

Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Halafu mwalimu mumoja wa Sheria akasimama na kumwuliza Yesu kwa kumupima: “Mwalimu, nifanye nini kusudi nipate uzima wa milele?”


Kisha akawapeleka inje na kuwauliza: “Wabwana wangu, inanipasa kufanya nini kusudi nipate kuokolewa!”


Nao watu waliposikia maneno hayo, wakachomwa katika mioyo yao na kuwaambia Petro na mitume wengine: “Wandugu zetu, tufanye nini?”


“Basi sasa ninawaweka chini ya ulinzi wa Mungu na wa neno lake la neema linaloweza kuwajenga katika imani na kuwapa urizi pamoja na watu wake wote watakatifu.


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Yesu na wanafunzi wake waliendelea hata wakafika kwenye kundi la watu. Pale mutu mumoja akamwendea Yesu, akapiga magoti mbele yake,


Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”


Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.


Munachunguza Maandiko Matakatifu, kwa maana munazani kuwa ndani yao mutapata uzima wa milele. Maandiko hayo ndiyo yanayonishuhudia,


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Walipomufikia, wakamwuliza: “Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mutu wa kweli. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu lakini unafundisha kwa ukweli njia Mungu anayoamuru kufuata. Utuambie basi, Sheria inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana? Ni sherti tulipe au hapana?”


Wakati Yesu alipoona watu wengi wanazidi kukusanyika mbiombio, akamukaripia yule pepo na kumwambia: “Wewe pepo wa bubu na wa kiziwi, ninakuamuru utoke ndani ya mutu huyu wala usimurudilie tena!”


Mutu mumoja mwenye ukoma alikuja kwa Yesu, akapiga magoti mbele yake na kumusihi, akisema: “Kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”


Basi wale wanawake wakaondoka upesi kutoka kwenye kaburi, wakijazwa na woga na furaha kubwa vilevile. Wakakimbia kwenda kuwapasha wanafunzi wake habari ile.


Na Kristo yeye mwenyewe alituahidi sisi uzima wa milele.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


Yesu akamwuliza: “Sababu gani unaniita mwema? Hakuna mutu anayekuwa mwema, isipokuwa Mungu peke yake.


Ninaomba Mungu aifungue mioyo yenu ipate kuona mwangaza wake. Kwa hiyo mutapata kujua tumaini munalokuwa nalo kutokana na mwito wa Mungu. Vilevile mupate kujua utajiri mukubwa wa urizi anaouwekea watu wake,


Ilifanyika vile, kusudi kwa neema yake tupate kuhesabiwa haki mbele ya Mungu na kuupata uzima wa milele tunaotumainia.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


na hivyo tutapata baraka zile ambazo Mungu aliwawekea watu wake. Baraka zisizoweza kuoza wala kuchafuka wala kupunguka; nazo zinawekewa akiba kwa ajili yenu mbinguni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite