38 Lakini Yesu akawajibu: “Twende pahali pengine katika vijiji vinavyokuwa karibu, kusudi nihubiri kule vilevile, kwa maana ni kwa ajili ya ile nimekuja.”
Lakini Yesu akawaambia: “Imenipasa kuhubiri Habari Njema ya Ufalme wa Mungu katika miji mingine vilevile, kwa maana ni kwa sababu ile nimetumwa.”
kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Mimi nimekutukuza wewe katika dunia kwa kuwa nimemaliza kazi ile uliyonipa.
Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”
Yesu akawajibu: “Kwa nini mulinitafuta? Hamujui kwamba ninapaswa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.
Nao walipomwona wakamwambia: “Watu wote wanakutafuta.”
Hivi akaenda fasi zote katika Galilaya, akihubiri katika nyumba za kuabudia na kufukuza pepo.