Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 1:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Watu wote wakashangaa sana na kuulizana: “Hatujaona mambo kama haya! Hakika mafundisho haya ni yenye mamlaka! Mutu huyu anaamuru hata pepo, nao wanamutii!”

Gade chapit la Kopi




Marko 1:27
15 Referans Kwoze  

Yesu akawakusanya wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapatia uwezo na mamlaka ya kufukuza pepo, na uwezo wa kuponyesha wagonjwa.


Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”


Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli.


Wakati Yesu alipokwisha kumufukuza yule pepo, yule bubu akaanza kusema. Nao watu wote wakashangaa na kusema: “Hatujaona jambo kama hili katika inchi yote ya Israeli!”


Watu wote wakashangaa sana na kusemezana: “Hatujaona mambo kama haya! Mutu huyu anawaamuru pepo kwa mamlaka na uwezo wake, nao wanatoka!”


Yesu na wanafunzi wake walipokuwa katika njia, wakipanda kwenda Yerusalema, yeye akatangulia mbele yao. Wanafunzi walishikwa na hofu, nao watu waliowafuata waliogopa. Yesu akawatwaa tena wanafunzi wake kumi na wawili, na kuanza kusemezana nao juu ya mambo yatakayomupata.


Wanafunzi wakashangaa sana kusikia maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena: “Watoto wangu, ni vigumu kabisa kuingia katika Ufalme wa Mungu!


Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena nina waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’, naye anakwenda. Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’, naye anakuja. Na nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’, naye anafanya vile.”


Yule pepo akamutikisa mutu yule kwa nguvu, akatoka ndani yake, akilalamika kwa nguvu.


Halafu sifa za Yesu zikaenea upesi katika jimbo lote la Galilaya.


Basi wakaingia ndani ya kaburi, na mule wakaona kijana mumoja akiikaa upande wa kuume, akivaa kanzu nyeupe. Nao wakashituka.


Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.


Halafu wakamukamata Paulo, na kumupeleka mbele ya Baraza Kubwa inayoitwa “Areopago,” wakamwuliza: “Unaweza kutujulisha maana ya mafundisho haya mapya unayotoa?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite