Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 1:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 “Kuna maneno gani kati yako na sisi, wewe Yesu wa Nazareti? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani: wewe ni Mutakatifu aliyetumwa na Mungu.”

Gade chapit la Kopi




Marko 1:24
25 Referans Kwoze  

Halafu wakaanza kulalamika wakisema: “Kuna maneno gani kati yako na sisi wewe Mwana wa Mungu? Umekuja hapa kwa kututesa mbele ya kutimia kwa wakati wetu?”


Si wewe unaamini kwamba kuna Mungu mumoja? Ni vizuri! Hata pepo wanaamini vile, nao wanatetemeka kwa woga.


akisema: “Ee Yesu wa Nazareti, kuna maneno gani kati yako na sisi? Ulikuja kutuangamiza? Ninakutambua wewe ni nani. Wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


Yeye alikuwa Mutakatifu na Mwenye Haki, lakini mukamukana, mukataka Pilato awafungulie mwuaji.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Filadelfia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayekuwa mutakatifu na mwenye ukweli, anayekuwa na ufunguo wa mufalme Daudi, anayefungua mulango wala hakuna anayeweza kuufunga, anayefunga wala hakuna anayeweza kuufungua.


maana hautaniachilia kubaki katika kuzimu, hautakubali mutumishi wako mutakatifu apate kuoza.


Wakati alipomwona Yesu, akalalamika na kuanguka mbele yake, na kusema kwa nguvu: “Yesu, Mwana wa Mungu Mukubwa, kuna neno kati yako na mimi? Ninakusihi, usinitese!”


na kulalamika kwa nguvu, akisema: “Yesu, Mwana wa Mungu Mukubwa, kuna neno kati yako na mimi? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”


Kweli wewe unanikinga na nguvu za kuzimu, haumwachi mutakatifu wako aone kaburi.


Na sasa tunaamini na kujua kwamba wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.


“Ndiyo, ni kweli mufalme Herode, naye mutawala Pontio Pilato walikusanyika katika muji huu pamoja na Waisraeli na watu wa mataifa mengine kwa kufanya shauri baya juu ya mutumishi wako mutakatifu Yesu, uliyemuchagua kuwa Kristo.


Naye akawauliza: “Ni mambo gani?” Nao wakamujibu: “Haujui mambo yaliyomupata Yesu wa Nazareti? Yeye alishuhudiwa na Mungu na watu wote kwamba alikuwa nabii mwenye uwezo katika mambo aliyofanya na kusema.


Kule akakaa katika muji ulioitwa Nazareti, kusudi yatimie maneno yaliyosemwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa mutu wa Nazareti.”


Halafu watu wote wa inchi ya Wagerasi wakashikwa na woga mukubwa, kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke kwao. Basi Yesu akaingia ndani ya chombo, kusudi apate kuondoka kule.


Hatukukuambia mambo haya tulipokuwa bado Misri? Tulikuambia utuache tuendelee kuwatumikia Wamisri. Ingalikuwa vizuri kuwatumikia Wamisri kuliko kukufia huku katika jangwa.”


Muda wa miaka saba mara makumi saba umewekwa kwa ajili ya watu wako na juu ya muji wako mutakatifu kwa kumaliza makosa, kukomesha zambi, kusamehe uovu, kuleta haki ya milele, kutia muhuri juu ya maono na unabii na kupakaa mafuta katika Pahali Patakatifu Sana.


Saa ile, mutu mumoja aliyeshikwa na pepo alikuwa ndani ya nyumba ya kuabudia. Akaanza kulalamika, akisema:


Yesu akamukaripia kwa nguvu, akimwamuru: “Nyamaza, na utoke ndani ya mutu huyu!”


Naye aliposikia kwamba Yesu wa Nazareti anapita katika njia ile, akalalamika, akisema: “Yesu Mwana wa Daudi, unisikilie huruma!”


Alipomwona Petro akiota moto, akamwangalia, na kumwambia: “Wewe vilevile ulikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”


Lakini kijana yule akawaambia: “Musishituke! Munamutafuta Yesu wa Nazareti aliyetundikwa juu ya musalaba. Yeye amefufuka, hayuko hapa. Muangalie, hapa ni pahali walipomuweka.


Lakini munajazwa na Roho Mutakatifu ambaye Kristo alimimia juu yenu, na kwa hiyo ninyi wote munajua ukweli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite