Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Alisema: “Wakati umetimia, na Ufalme wa Mungu ni karibu! Mugeuke toka zambi zenu na kukubali Habari Njema!”

Gade chapit la Kopi




Marko 1:15
17 Referans Kwoze  

akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Tangia wakati huo Yesu akaanza kuhubiri, akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Kusudi la mupango ule utakaotimia kwa wakati uliowekwa, ni kukusanya viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia chini ya utawala wa Kristo.


Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Muponyeshe wagonjwa wanaokuwa mule na kuwaambia wakaaji: ‘Ufalme wa Mungu umewakaribia ninyi.’


Mutakapokuwa mukienda, muhubiri kwa watu kwamba Ufalme wa mbinguni umekaribia!


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


‘Tunawakungutia ninyi hata mavumbi ya muji wenu toka juu ya miguu yetu kuwa ushuhuda juu yenu. Na hata hivi mujue vizuri kwamba Ufalme wa Mungu umewakaribia.’


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Lakini sasa yamefunuliwa na maandiko ya manabii kufuatana na amri ya Mungu wa milele, kusudi mataifa yote yapate kumwamini na kumutii.


aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.


Alifunua neno lake kwa wakati alioupanga kwa njia ya mahubiri ambayo yeye Mungu Mwokozi wetu aliyoniamuru kutangaza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite