Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Nyuma ya kutiwa kwa Yoane katika kifungo, Yesu alikwenda Galilaya, akahubiri Habari Njema inayotoka kwa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Marko 1:14
16 Referans Kwoze  

Yesu alizunguka katika Galilaya yote akifundisha katika nyumba zao za kuabudia, akihubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha watu waliokuwa na magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


Yesu aliposikia kwamba Yoane ametiwa katika kifungo, akaenda zake Galilaya.


Hivi, Kristo amekuja kutangaza Habari Njema ya amani kwa ninyi watu wa mataifa mengine, muliokuwa mbali na Mungu, na kwa Wayuda waliokuwa karibu naye.


Nyuma ya pale Yesu akapita katika miji na vijiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza Habari Njema ya Ufalme wa Mungu. Wale wanafunzi wake kumi na wawili walienda naye


Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.


Yesu alizunguka katika miji na vijiji vyote, akiwafundisha watu katika nyumba zao za kuabudia, akiwahubiri Habari Njema ya Ufalme. Aliponyesha magonjwa yote na uzaifu wa kila namna.


“Nilikuwa nikizungukazunguka kati yenu ninyi wote nikitangaza Ufalme wa Mungu. Lakini sasa, ninajua kwamba hakuna hata mumoja atakayeniona tena.


Halafu akawaambia wasimamizi waliokuwa chini yake: “Mutu huyu ni Yoane Mubatizaji aliyefufuka! Ni kwa sababu hii amepata uwezo wa kufanya miujiza.”


Lakini Herode akaongeza ubaya mwingine kwa kumutia Yoane ndani ya kifungo.


Yoane Mubatizaji, akiwa katika kifungo, akapata habari za mambo Kristo aliyokuwa akifanya. Basi akawatuma wanafunzi wake


Tangia wakati huo Yesu akaanza kuhubiri, akisema: “Mugeuke toka zambi zenu, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia!”


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo, mutumishi wa Kristo Yesu, niliyeitwa na Mungu kuwa mutume na niliyewekwa kwa kazi ya kutangaza Habari Njema yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite