Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Marko 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”

Gade chapit la Kopi




Marko 1:11
19 Referans Kwoze  

Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Halafu wingu likatokea na kuwafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Mufalme anasema: “Nitatangaza amri ya Yawe. Mungu aliniambia: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo nimekuwa baba yako.


Kwa maana yeye ametuokoa toka katika uwezo wa giza, na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mupendwa,


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Na Baba aliyenituma amenishuhudia vilevile. Ninyi hamujasikia sauti yake wakati wowote wala hamujaona sura yake.


Mimi nimeona mambo haya, nami ninashuhudia kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”


Na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu niliyemuchagua. Mumusikilize!”


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Na sasa tunaamini na kujua kwamba wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


“Muangalie, mutumishi wangu niliyejichagulia, anayekuwa mupendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitamujaza Roho wangu, naye atatangaza haki yangu kwa mataifa.


Mara moja wakati Yesu alipotoka ndani ya maji, akaona mbingu zinafunguka na Roho Mutakatifu akishuka juu yake kwa mufano wa njiwa.


na Roho Mutakatifu akashuka juu yake katika hali ya kimwili kwa mufano wa njiwa. Na sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite