Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Babu zetu walitenda zambi na sasa hawako tena; nasi tunabeba makosa yao.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 5:7
15 Referans Kwoze  

Siku hizo watu hawatasema tena: Wazee walikula matunda mabichi ya mizabibu, na meno ya watoto ndiyo yanaumizwa.


Ninyi mumefanya vibaya zaidi kuliko babu zenu, maana kila mumoja wenu ni mwenye moyo mugumu na mwenye nia mbaya, wala hamunisikilizi.


Kwa nini munarudiliarudilia mezali hii katika inchi ya Waisraeli: Wababa wamekula matunda mabichi ya mizabibu, lakini ni meno ya watoto wao ndiyo yanaumizwa!


Tunakubali uovu wetu, ee Yawe, tunakubali uovu wa babu zetu, maana, tumekukosea wewe.


Usiiname mbele yao wala kuvitumikia, kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu. Ninawaazibu wana kwa ajili ya maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha ine cha wale wanaonichukia.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


Baba yao Yakobo, akawaambia: “Munaniondolea watoto wangu! Yosefu hayuko, Simeoni hayuko, sasa munataka kumutwaa Benjamina. Hayo yote yanaanguka juu yangu!”


Babu zenu, wako wapi? Na manabii, wanaishi milele?


Mbona haunisamehe kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi kisha muda kidogo nitalazwa chini katika mavumbi. Utanitafuta, lakini sitakuwa tena!


Anayeniona sasa, hataniona tena, mara tu ukiniangalia nitakuwa nimetoweka.


Wakamwambia: “Sisi, watumishi wako, tuko wandugu kumi na wawili, wana wa mutu mumoja, mwenyeji wa inchi ya Kanana. Mudogo wetu amebaki na baba kwa nyumba na ndugu yetu mwingine ni marehemu.”


“Mimi Yawe si mwepesi wa hasira, ni mwenye wema mwingi, na ni mwenye kusamehe uovu na makosa. Lakini kwa vyovyote vile sitakosa kuwaazibu watoto na wajukuu mpaka kizazi cha tatu na cha ine kwa zambi za wazazi wao.”


Nawe utawajibu hivi: Babu zenu waliniacha. Wakafuata miungu mingine, wakaitumikia na kuiabudu. Waliniacha, wala hawakuzitii sheria zangu.


Azabu ya uchafu wa tabia na machukizo yako utaibeba wewe mwenyewe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite