20 Sababu gani umetusahau kwa muda murefu hivyo na kutuacha siku nyingi hivyo?
Amuka, ee Bwana! Mbona umelala? Inuka! Tafazali usitutupe milele!
Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Daudi.
Umezipunguza siku za ujana wake, ukamufunika haya tele.
Utustareheshe tena, ee Mungu mwokozi wetu; uondoe chuki unayokuwa nayo juu yetu.
Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?
Mashairi ya Asafu. Kwa nini, ee Mungu, umetutupilia kabisa? Mbona hasira yako inawaka juu ya kondoo wako?
Juu ya kuta zako, ee Yerusalema, nimeweka walinzi, usiku na muchana hawatakaa kimya hata kidogo. Enyi munaomukumbusha Yawe ahadi yake, musikae kimya;
Mpaka wakati gani, ee Yawe, utaendelea kunisahau? Mpaka wakati gani utanificha uso wako?
Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”
Wewe Sayuni unasema: Yawe ameniacha. Hakika Bwana wangu amenisahau.
Namna gani unakuwa kama mutu aliyechanganyikiwa, kama shujaa asiyeweza kusaidia mutu? Ingawa hivyo wewe ee Yawe unakaa katikati yetu; nasi tunajulikana kwa jina lako, usituache.