Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 5:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Inchi yetu imepewa kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wengine.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 5:2
13 Referans Kwoze  

Utajiri wao utanyanganywa, na nyumba zao zitaachwa tupu! Watajijengea nyumba, lakini hawataishi humo. Watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.


Inchi yenu imeharibiwa kabisa; miji yenu imeteketezwa kwa moto. Wageni wamebeba mazao ya inchi yenu mbele ya macho yenu, imeharibiwa kama vile Sodoma.


Nitaleta watu wa mataifa mabaya sana nao watarizi nyumba zao. Nitakikomesha kiburi chao, na pahali pao pa kutambikia patachafuliwa.


Utajiri wao nitautia katika mikono ya mataifa mengine; watu waovu wa dunia wataunyanganya na kuuchafua.


Nyumba zao zitapewa watu wengine, nayo mashamba yao na wake zao vilevile; maana nitaunyoosha mukono wangu, kuwaazibu wakaaji wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe.


Sisi watakatifu wako tulirizi inchi kwa muda kidogo tu, lakini waadui zetu wakakuja wakaharibu hekalu lako.


Wana-kondoo watakula majani kule, kama vile katika shamba la kuwakulishia. Wana-mbuzi wanono watatafuta chakula chao kule kule.


Anayemudai kitu amunyanganye mali yake yote, na wageni wakule mapato ya jasho lake!


Itawabidi kuiacha hiyo inchi yenu niliyowapa, nami nitawafanya muwatumikie waadui zenu katika inchi musiyoijua, kwa sababu hasira yangu imewaka kama moto usiozimika hata milele.


Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.


Waisraeli wamemezwa, wanakuwa kati ya mataifa mengine, kama chombo kisichokuwa na faida yoyote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite