Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 5:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini wewe Yawe unatawala milele, kiti chako cha kifalme kinadumu kwa vizazi vyote.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 5:19
23 Referans Kwoze  

Maisha yangu ni kama kivuli cha magaribi; ninanyauka kama majani.


Mishale yako ni mikali, inapenya mioyo ya waadui za mufalme; nayo mataifa yanaanguka chini yako.


Ufalme wako ni ufalme wa milele; mamlaka yako yanadumu vizazi vyote. Yawe ni mwaminifu katika ahadi zake zote, ni mwema katika matendo yake yote.


Waadui wameangamia milele; umeiongoa miji yao, ukumbusho wao umetoweka.


Bwana Mungu Mwenye Uwezo anasema: “Mimi ni Alfa na Omega.” Ni yeye anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Yesu Kristo ni yule yule, jana, leo na hata milele.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Yawe anatawala milele. Mungu wako, ee Sayuni, ni mufalme kwa vizazi vyote! Haleluia!


Mbele milima haijakuwa, mbele haujauumba ulimwengu, wewe ndiwe Mungu, milele na milele.


Ufalme, utawala na ukubwa wa falme zote katika dunia watapewa kwa watu wa watakatifu wa Mungu Mukubwa. Ufalme wao utakuwa wa kudumu milele, na tawala zote zitawatumikia na kuwatii.


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Wakati wa wafalme wale, Mungu wa mbinguni ataanzisha ufalme ambao hautaangamizwa hata kidogo. Watu wengine hawataushinda na kuutawala ufalme huo, lakini ufalme huo utaziponda na kuzikomesha falme zilizotangulia, nao utadumu milele.


Yawe ameikaa juu ya mafuriko ya maji; Yawe ni mufalme anayetawala milele.


Yawe ni mufalme milele na milele! Mataifa yatatoweka katika inchi yake.


Mungu wa milele ndiye kimbilio lenu; nguvu yake inaonekana katika dunia. Aliwafukuza waadui mbele yenu; aliwaamuru: ‘Muwaangamize.’


Ni mimi Yoane ninayewaandikia ninyi makanisa saba munaokuwa katika jimbo la Azia. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja, na kutoka kwa roho saba wanaokuwa mbele ya kiti chake cha kifalme,


Yesu akageuka, akawaona wakimufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakajibu: “Rabi (maana yake ‘Mwalimu’), unakaa wapi?”


Kiti chako cha kifalme ni imara tangu zamani; wewe umekuwa mbele ya nyakati zote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite