8 Sasa sura zao ni nyeusi kuliko makaa, wanapita katika barabara bila kujulikana; ngozi yao imebanana na mifupa yao, imekauka, imekuwa kama kuni.
Ngozi zetu zinawaka moto kama furu, kwa sababu ya njaa inayotuchoma.
Ngozi yangu inakuwa nyeusi na inachubuka, mifupa yangu inaungua kwa homa.
Nimekunjamana kama mufuko wa ngozi katika moshi, hata hivyo sijasahau masharti yako.
Mwili wangu umebakia tu mifupa na ngozi, nimeponyoka kisha kupoteza yote.
Munyanganye feza, munyanganye zahabu! Mali yake haina mwisho! Kuna wingi wa kila kitu cha bei kali!
Wanapokaribia, watu wanajaa hofu, nyuso zao zinawaivya.
Wengi waliomwona walishituka, kwa vile sura yake ilikuwa imeharibika; hakukuwa tena na umbo la mwanadamu!
kwa sababu ya kasirani na hasira yako, maana umeniokota na kunitupilia mbali.
Mishale yako imenichoma; mukono wako umenigandamiza.
Muchana na usiku mukono wako ulinilemea; nguvu zangu zikakwisha, kama maji yanavyokauka wakati wa kipwa.
Mwili wake unakonda hata hawezi kutambuliwa, na mifupa yake iliyofichama ikatokea inje.
Walipomwona kwa mbali hawakumutambua. Basi, wakaanza kulalamika na kulia. Wakapasua nguo zao, wakarusha mavumbi katika anga na juu ya vichwa vyao.
‘Tunawakungutia ninyi hata mavumbi ya muji wenu toka juu ya miguu yetu kuwa ushuhuda juu yenu. Na hata hivi mujue vizuri kwamba Ufalme wa Mungu umewakaribia.’