Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa kuliko zambi za watu wa Sodoma, muji ambao uliteketezwa kwa rafla bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 4:6
14 Referans Kwoze  

akaiangamiza miji hiyo, bonde lote, wakaaji wake wote na mimea yote katika inchi hiyo.


Ninawaambia hakika kwamba kwa Siku ya hukumu muji ule utaazibiwa vikali zaidi kuliko muji Sodoma.”


“Mutumishi anayejua mapenzi ya bwana wake, lakini anakosa kujiweka tayari na kutofanya sawa na mapenzi ya bwana yule, atapigwa fimbo nyingi.


Kwa maana katika siku zile kutakuwa mateso makubwa yasiyotokea tangia kuumbwa kwa dunia mpaka sasa, wala hakutatokea tena mateso kama yale.


Umetimiza yale uliyosema utatutendea sisi pamoja na watawala wetu kwa kuuazibu Yerusalema vikali zaidi ya muji mwingine wowote katika dunia.


Afazali waliouawa kwa upanga kuliko waliokufa kwa njaa, ambao walikufa polepole kwa kukosa mazao ya shamba.


Halafu Yawe akateremusha moto mukali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,


Mutu huyo akuwe kama miji Yawe aliyoiangusha bila huruma. Mutu huyo asikie kilio asubui, na muchana asikie kelele za vita,


Kila mutu atapatwa na mambo yaleyale: mutu wa kawaida na kuhani; mutumwa na bwana wake; mujakazi na bibi wake; mwenye kununua na mwenye kuuzisha; mukopeshaji na mukopaji; mwenye kudai na mwenye kudaiwa.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


Kwa werevu wake, atafanikiwa katika mipango yake ya udanganyifu, naye atajitukuza. Atawaangamiza watu wengi sana, na atataka kupigana na Mukubwa wa wakubwa, lakini ataangamizwa pasipo kutumia nguvu za kimutu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite