Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 4:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Tulichoka kukaa macho kungojea musaada; tulikesha na kungojea kwa hamu taifa ambalo halikuweza kutuokoa.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 4:17
15 Referans Kwoze  

Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na Waisraeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea inchi ya Misri. Waisraeli watatambua kwamba mimi ni Bwana wao Yawe.


Kisha wote waliotegemea Kushi na kujivunia Misri watajuta na kufazaika.


Mufalme wa Misri hakutoka tena katika inchi yake, kwa sababu mufalme wa Babeli alinyanganya inchi yote iliyokuwa mali ya Misri pale zamani, tangia kwenye kijito cha Misri mpaka kwenye muto Furati.


Niliwaita wapenzi wangu, lakini wao wakanidanganya. Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji, wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.


Unapokuwa sasa mabomoko matupu, Yerusalema unakumbuka utukufu wake. Ulipoangukia katika mikono ya waadui zake, hakuna aliyekuwa pale kwa kuusaidia. Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.


Wakati wa mavuno umepita, nao wakati wa jua kali umekwisha, nasi hatujaokolewa!


Kwa nini unaniachilia hivi, ukibadilishabadilisha mwenendo wako? Utafezeheshwa na Misri kama ulivyofezeheshwa na Asuria.


Na sasa itakufalia nini kwenda Misri kunywa maji ya muto Nili? Au itakufalia nini kwenda Asuria kunywa maji ya muto Furati?


Halafu agano lenu na kifo litavunjika, na mapatano yenu na kuzimu yatafutwa. Ile hasara kubwa itakapokuja itawaangusha chini.


Na huko vilevile utatoka na haya, mikono ikiwa juu ya kichwa. Mimi Yawe nimewakataa wale uliowategemea, wala hautafanikiwa kwa musaada wao.


Tumewanyooshea Wamisri na Waasuria mikono, kusudi tupate chakula cha kutosha.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite