Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 4:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wamama ambao wanakuwa na huruma kubwa, waliwapika watoto wao wenyewe, wakawafanya kuwa chakula chao, wakati watu wangu walipoangamizwa.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 4:10
12 Referans Kwoze  

Angalia, ee Yawe, uone! Kuna yeyote uliyemutendea kama ulivyotutendea sisi, hata wamama wawakule watoto wao nao makuhani wauawe ndani ya hekalu lako?


Lakini Yawe anasema: Munafikiri kwamba mama anaweza kumusahau mutoto anayemunyonyesha, wala kumuchukia mutoto wa tumbo lake? Hata kama mama anaweza kumusahau mutoto wake, mimi sitakusahau hata kidogo.


Waadui wao wanavizia maisha yao watauzunguka muji ule kwa vita. Wataleta taabu na masumbuko hata watu watakula wenzao. Nitawafanya wakule miili ya wana na wabinti zao.


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


Hata mbweha wanatoa maziwa, na kuwanyonyesha watoto wao; lakini watu wangu wamekuwa wabaya, wanafanya kama mbuni katika jangwa.


Macho yangu yanabubujika mito ya machozi kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu.


Halafu mutakula watoto wenu, wanaume na wanawake.


Katika siku ya tisa ya mwezi wa ine njaa ilikuwa kali sana katika muji hata hakukuwa chakula chochote kwa ajili ya wakaaji wake.


Macho yangu yamevimba kwa kulia, roho yangu imechafuka, moyo wangu una huzuni nyingi, kwa sababu ya kuangamizwa kwa watu wangu, kwa sababu watoto wachanga na wale wanaonyonya wanazimia katika barabara za muji.


Kwa nini munapiga kelele za shangwe, na muji wote umechangamuka na kujaa vigelegele? Watu wenu waliokufa hawakuuawa katika vita, wala hawakuuawa katika mapigano.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite