Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 3:40 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

40 Tupime na kuchunguza mwenendo wetu tupate kumurudilia Yawe.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 3:40
22 Referans Kwoze  

Mujichunguze ninyi wenyewe kusudi mupate kujua kama munasimama imara katika imani. Mujipime. Si munajua kwamba Yesu Kristo anakaa kati yenu? Kama si vile ni kusema kwamba mumeshindwa.


Nimefikiri juu ya mwenendo wangu, na nimerudi nifuate maagizo yako.


Mujue kwamba Yawe amejichagulia mutu wake wa haki. Yawe anasikia kila mara ninapomwomba.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.


Basi kila mutu ajichunguze mwenyewe na kisha akule mukate huu na kunywa kikombe hiki.


Lakini tungejichunguza sisi wenyewe kwanza, hatungehukumiwa na Mungu.


Kwa hiyo wajumbe wakapita katika inchi yote ya Israeli na ya Yuda kwa kupeleka barua zile kufuatana na amri ya mufalme na wakubwa wake. Barua hizo zilikuwa na ujumbe huu: “Enyi watu wa Israeli muliobaki nyuma ya mashambulizi ya wafalme wa Asuria. Mumurudilie Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, kusudi naye apate kuwarudilia.


Kwa sababu amefikiri, akaachana na makosa aliyoyafanya, hakika ataishi; hatakufa.


Mukimurudilia Yawe, wale ambao walipeleka wandugu zenu na watoto wenu kuwa wafungwa, watawahurumia na kuwaacha warudi katika inchi hii. Kwa maana Yawe, Mungu wenu, ni mwenye huruma na rehema, naye hatawageuzia mugongo ikiwa mutamurudilia.”


Mambo haya yote yatakapowapata huko, kisha mukipata taabu, mutamurudilia Yawe na kumutii.


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


Yawe wa majeshi, Yawe, ndilo jina lake.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite