Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 3:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 wanapomunyima mutu haki katika tribinali, basi, Yawe haoni hayo?

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 3:36
8 Referans Kwoze  

Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?


Ukweli umekosekana, naye anayeacha uovu ananyanganywa. Mungu aliona mambo hayo. Alichukizwa kwamba watu hawafuati sheria yake.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Muda wa kufunga kilio ulipokwisha, Daudi aliagiza wamulete Batiseba na kumupeleka katika nyumba yake. Batiseba akakuwa muke wa Daudi, naye akamuzalia Daudi mutoto mwanaume. Lakini jambo hilo Daudi alilofanya lilimuchukiza Yawe.


“Ikiwa kuna ugomvi kati ya watu wawili, na wakienda kwa tribinali kuamua maneno yao, mumoja akionekana hana kosa, na mwingine akihukumiwa,


Wanaangamiza watu wako, ee Yawe, wanawagandamiza hao wanaokuwa mali yako.


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Uliuona uovu niliotendewa, ee Yawe; uniamulie kwa wema maneno yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite