3 Amenyoosha mukono wake juu yangu mimi tu, akiniazibu tena na tena muchana kutwa.
Lakini wao waliasi, wakaihuzunisha roho yake takatifu. Basi, Mungu akageuka, akakuwa adui yao; yeye mwenyewe akapigana nao.
Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.
Nitapigana nawe; nitayeyusha uchafu wako kabisa, na kuondoa takataka yako yote.
Kama nimekunjia yatima ngumi katika tribinali nikijua nitapendelewa na waamuzi,
Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.
Ee Yawe, usiniazibu kwa hasira yako, usiniadibishe kwa kasirani yako.
Mishale ya Mungu Mwenye Uwezo imenichoma; nafsi yangu imekunywa sumu yake. Vitisho vya Mungu vimenipata.
Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja. Alinikamatia katika shingo na kunipasua vipandevipande. Akanifanya shabaha ya mishale yake,
Munionee huruma, munionee huruma, enyi warafiki zangu; maana mukono wa Mungu umenigusa.