Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 3:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Inamupasa kuinama na kujinyenyekeza, labda tumaini litakuwa likingali.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 3:29
12 Referans Kwoze  

Mimi sifai kitu. Nitakujibu nini? Ninafunga kinywa changu.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Mutafute Yawe, enyi wanyenyekevu wote katika inchi, enyi munaozitii amri zake. Mutafute haki, mutafute unyenyekevu; labda mutaiponyoka siku ya kasirani ya Yawe.


Labda Mungu atabadilisha nia yake, na kuacha kutukasirikia, nasi hatutaangamizwa!


Labda Yawe, Mungu wenu, atabadilisha nia na kuwapa baraka ya mazao, mutaweza kumutolea sadaka za chakula na kinywaji.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Kuna matumaini kwa siku zenu zinazokuja, maana watoto wenu watarudia katika inchi yao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wakati alipokuwa katika taabu, akamwomba Yawe, Mungu wake rehema. Akajinyenyekeza sana mbele ya Mungu wa babu zake.


Nimejishonea nguo za gunia; utukufu wangu nikautupa katika mavumbi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite