28 Heri kwa mutu kukaa peke yake na kimya, mambo mazito yanapomupata kutoka kwa Mungu.
Mimi sikuikaa pamoja na wanaojifurahisha, wala sikufurahi pamoja nao. Niliikaa peke yangu nikilemewa na nguvu yako; kwa maana ulinijaza hasira yako.
Wazee wa Sayuni wameikaa chini kimya, wamejitia mavumbi juu ya vichwa na kuvaa gunia. Wabinti wa Yerusalema wameinamisha vichwa chini.
Nimekuwa kama ndege katika jangwa, kama bundi kwenye matongo.
Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.
Ni vizuri kwa mutu kujifunza uvumilivu tangu wakati wa ujana wake.
Hata leo malalamiko yangu ni ya uchungu. Ninapata maumivu na kuugua.
Niko kama bubu, sisemi kitu, kwa maana wewe ndiwe uliyetenda hayo.