Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ameivunja kwa hasira nguvu yote ya Israeli. Hakunyoosha mukono kwa kuwasaidia walipokutana na adui; amewawakia watu wa Yakobo kama moto, akateketeza kila kitu.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:3
25 Referans Kwoze  

Mbona umeficha mukono wako wa kuume? Kwa nini haunyooshi mukono na kuwapiga?


Kwa hiyo aliwamwangia kasirani yake kali, akawaacha kupatwa na vita kali. Hasira yake iliwawakia kila upande, lakini wao hawakuelewa chochote; iliwachoma, lakini hawakufikiri juu ya jambo hilo.


Lakini mimi nitafurahi milele, nitamwimbia Mungu wa Yakobo sifa.


Ninawaambia wenye kiburi: ‘Mwache kiburi’, na waovu: ‘Musiote mapembe!


Nguvu za Moabu zimevunjika na uwezo wake umevunjika. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Umezipunguza siku za ujana wake, ukamufunika haya tele.


Ee Yawe, utakasirika hata milele? Hasira yako itawaka kama moto hata wakati gani?


Anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”


Ametuletea Mwokozi mwenye uwezo, toka ukoo wa mutumishi wake Daudi.


Nitawaazibu kadiri ya matendo yenu. Nitawakisha moto katika pori lenu nao utateketeza kila kitu kinachokuwa kando yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.


Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Wenye nguvu watakuwa kama majani yenye kukauka, matendo yao yatakuwa kama cheche za moto. Watateketea pamoja na matendo yao, wala hakutakuwa mutu wa kuwaokoa.


Humo nitamuchipukiza mufalme shujaa wa ukoo wa Daudi. Kama vile taa inayowaka, nitamwimarisha mufalme niliyemuchagua.


Mimi nitawaponda wapinzani wake; nitawaangamiza wote wanaomuchukia.


Nimejishonea nguo za gunia; utukufu wangu nikautupa katika mavumbi.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


Kwa sababu wameniacha mimi na kufukizia miungu mingine ubani kusudi wanikasirikishe sana kwa kazi zote za mikono yao, basi kasirani yangu itamwagika juu ya pahali hapa wala haitatulizwa.


Aliteremusha moto kutoka juu, ukanichoma hata ndani ya mifupa yangu. Alinitegea wavu akaninasa, kisha akanirudisha nyuma, akaniacha peke yangu na kuzimia muchana kutwa.


Yawe ameonyesha kabisa kasirani yake, aliimwanga hasira yake kali, aliwasha moto huko katika Sayuni ambao uliteketeza misingi yake.


Baragumu imepigwa na kuwafanya wote wakuwe tayari. Lakini hakuna anayekwenda kwa vita, kwa maana kasirani yangu iko juu ya watu wote.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema: Kwa kasirani yangu nitazusha upepo wa zoruba na mvua nyingi ya mawe, navyo vitauangusha ukuta huo.


Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite