Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Umewaalika kama kwenye sikukuu waadui zangu walionitisha kila upande. Katika siku ya hasira yako, ee Yawe, hakuna aliyetoroka au kubakia. Wale niliowazaa na kuwalea, waadui zangu wamewaangamiza.

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:22
16 Referans Kwoze  

Hatuwezi kwenda katika mashamba, wala kutembea katika barabara; waadui wameshika silaha katika mikono, vitisho vimejaa kila pahali.


Nimesahaulika kama mutu aliyekufa; nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.


Lakini mbona ninawaona wametishwa? Wamerudi nyuma. Mashujaa wao wamepigwa, wamekimbia mbio, bila hata kuangalia nyuma. Kuna kitisho kila upande. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kesho yake asubui, Pashuri akamufungua Yeremia toka minyororo ile. Yeremia akamwambia hivi: Yawe hakuiti tena jina lako “Pashuri”, lakini “Kitisho Kila Pahali”.


Watoto wenu watalaaniwa na mazao yenu ya inchi; mifugo yenu italaaniwa isiongezeke.


Kila mara itakapopita kwenu itawapata; nayo itapita kila asubui, muchana na usiku. Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Nitaleta hasara juu yao ambayo hawataweza kuiepuka. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza.


Sasa, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Mbona munajiletea maovu makubwa namna hii, na kujiangamiza ninyi wenyewe, wanaume kama vile wanawake, watoto wadogo na wachanga, hata kusibaki mutu katika inchi ya Yuda?


Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.


Ee Yawe, umekataa Yuda kabisa? Moyo wako umechukizwa na Sayuni? Kwa nini umetupiga vibaya kama hivi, hata hatuwezi kupona tena? Tulitazamia kupata amani, lakini hakuna kitu kizuri. Tulitazamia kupona, lakini tumepatwa na vitisho.


Kisha, wewe Zedekia, mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wa muji huu ambao watakaoponyoka magonjwa hayo makali pamoja na vita na njaa, nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli na katika mikono ya waadui zenu wanaovizia maisha yao. Nebukadneza atawaua kwa upanga wala hatawahurumia au kuwaachilia au kuwasamehe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite