Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Maombolezo 2:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Angalia, ee Yawe, uone! Kuna yeyote uliyemutendea kama ulivyotutendea sisi, hata wamama wawakule watoto wao nao makuhani wauawe ndani ya hekalu lako?

Gade chapit la Kopi




Maombolezo 2:20
24 Referans Kwoze  

Wamama ambao wanakuwa na huruma kubwa, waliwapika watoto wao wenyewe, wakawafanya kuwa chakula chao, wakati watu wangu walipoangamizwa.


Waadui wao wanavizia maisha yao watauzunguka muji ule kwa vita. Wataleta taabu na masumbuko hata watu watakula wenzao. Nitawafanya wakule miili ya wana na wabinti zao.


Makuhani wao walikufa kwa upanga, wala wajane wao hawakuomboleza.


Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake na makosa ya makuhani wake, ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.


Nikamwomba Yawe, nikisema: Ee Yawe, usiwaangamize watu wako na urizi wako, watu uliowakomboa na kuwatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo na nguvu yako kubwa.


Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


Yawe mwenyewe aliwatawanya, wala hatawajali tena. Makuhani hawaheshimiwi tena, wazee hawapendelewi tena.


Niliwaita wapenzi wangu, lakini wao wakanidanganya. Makuhani na wazee wangu wamekufia katika muji, wakijitafutia chakula kusudi wajirudishie nguvu zao.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Halafu mutakula watoto wenu, wanaume na wanawake.


Kwa nini munapiga kelele za shangwe, na muji wote umechangamuka na kujaa vigelegele? Watu wenu waliokufa hawakuuawa katika vita, wala hawakuuawa katika mapigano.


Kwa hiyo, Yawe alimuleta mufalme wa Wakaldea ambaye aliwaangamiza vijana wao kwa upanga hata ndani ya Pahali Patakatifu; wala hakumuhurumia mutu yeyote akuwe kijana au binti, muzee au muzaifu. Wote Yawe aliwatia katika mikono yake.


Kisha, wewe Zedekia, mufalme wa Yuda, pamoja na wakubwa wa serikali yako na watu wa muji huu ambao watakaoponyoka magonjwa hayo makali pamoja na vita na njaa, nitawatoa katika mikono ya Nebukadneza, mufalme wa Babeli na katika mikono ya waadui zenu wanaovizia maisha yao. Nebukadneza atawaua kwa upanga wala hatawahurumia au kuwaachilia au kuwasamehe. –Ni ujumbe wa Yawe.


Akawaambia: Muchafue nyumba ya Yawe kwa kuvijaza viwanja vyake maiti, kisha musonge mbele. Basi, wakaenda, wakawaua watu katika muji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite